Jumapili, 15 Machi 2015

HUDUMA YA KINABII


Manabii
(Prophetes)
Neno nabii limetokana na maneno
haya “Pro ” yaani mbele, na
“ Phemi ” yaani kujulisha wazo la
Mungu au mtu, lisilojulikana.
Manabii husema mambo ya mbele
na pia ya sasa kwa uvuvio wa
Roho Mtakatifu. Kwa maana ya
pili niliyoisema hapo juu,
Mchungaji mwalimu au mwinjilisti
asemapo Neno wakati wa sasa kwa
msukumo na ufunuo wa Roho
Mtakatifu, asemapo Neno hilo la
wakati, husimama kama nabii kwa
wakati huo.
HALI HIZI IKIWA ZINADUMU
KWA MTU KATIKA HUDUMA
INAWEZEKANA NI NABII AU ANA
HUDUMA YA KINABII
(a) Nabii ni mtu awezaye kujua
wazo la Mungu la wakati na
kulisema au kulitenda.
Anaweza kuwa haitwi nabii,
lakini hali hii ni ya kinabii.
(b)  Nabii anapewa neema ya kujua
wazo la moyo wa mtu na
kulisema (Matendo 5:3). Mara
nyingine wazo la Mungu
kuhusu mtu, watu au hali ya
nchi na anga la kiroho.
(c) Mungu humpa kujua ayaonayo
Yeye (Mungu) wakati ujao,
wakati wa sasa au wakati
uliopita (Matendo 11:27-30).
(d) Manabii hutengeneza misingi
iliyoharibika na kuimarisha
misingi kwa njia ya kufundisha
neno la Mungu kwa ufunuo
wa Roho. Huduma ya
mwalimu afundishaye neno la
wakati kwa ufunuo wa Roho
inaweza kuitwa mwalimu wa
kinabii.
(e) Katika Agano jipya nabii
hufanya kazi katika timu ya
huduma, sio peke yake,
hufanya na viongozi wengine
katika huduma tano. Huyu
siye mtu mmoja aliyejuu na
wengine wote wako chini yake
wakisubiri Mungu aseme
kupitia yeye tu, mfumo huu
sio wa Agano Jipya. Katika
Agano Jipya manabii hufanya
kazi katika timu (Matendo
13).
(f)   Karama kuu katika huduma ya
nabii ni neno la maarifa,
unabii, neno la hekima,
kupambanua roho, mara
nyingine karama za nguvu
kama miujiza, uponyaji na
imani maalum. Kuna tofauti
kati ya huduma ya nabii na
karama ya unabii, mtu
akitumiwa katika karama ya
unabii haimfanyi yeye kuwa
nabii.
(g) Mara nyingine huduma ya
nabii hujificha katika huduma
nyingine. Kwa mfano mtu
anaweza kuwa mwalimu,
mchungaji au mwinjilisti na
hapo hapo ni nabii. Mfano wa
mtu wa namna hii ni askofu
Immanuel Lazaro.
(h) Manabii hupambanua nyakati
za kiungu na majira ya jambo
kufanyika na kuwaandaa watu
(Matendo 11:28, Matendo
21:10-11).
(i) Kila nabii ni mwombaji, lakini
si kila mwombaji ni nabii
(Yeremia 27:18). Haiwezekani
kuwa nabii bila kuwa
mwombaji, ila inawezekana
kuwa mwombaji bila kuwa
nabii.
(j) Utendaji kazi wa kinabii upo
tofauti tofauti. Kuna manabii
waalimu (Kenneth Haggin),
manabii wainjilisti(Charles
Finney), manabii wachungaji,
manabii mitume na manabii
walio manabii tu. Kuna
manabii waimbaji, pia
waombaji manabii. Wakati
wanaomba huona jambo na
kulibadilisha kwa mamlaka au
kulisimamisha kwa mamlaka.
(k) Neno la kinabii linaposemwa
ni vema lizalishwe katika
ulimwengu wa mwili kwa
maombi na maombezi, maana
adui hujaribu kuzuia kusudi
ka Mungu lililonenwa kinabii.
Mfano mtoto aliyetabiriwa
kuwa mtumishi, Neno hilo
latakiwa liatamiwe kwa
maombezi limtokee.
(l) Manabii na maneno ya kinabii
hujidhihirisha wakati maalum
( Kairos) na si wakati wote wa
masaa ishirini na nne
( Kronos). Katika Agano Jipya
huduma hii haionekani sana
pengine ni kwasababu ya
udhihirisho wa Roho
Mtakatifu na sauti ya Mungu
kwa kila mwamini.
(m)Nabii akitoa neno katika kundi
wajibu wake huisha. Wajibu
unaofuata ni wa mchungaji,
mwalimu au mtume kulithibitisha
na kulijaribu kwa maandiko na
kulihakikisha, hata kama ni Mungu
anasema (1Wathesalonike
5:20-21). Maandiko yana mamlaka
ya mwisho kuliko neno la kinabii.
Nabii lazima ajitiishe chini ya
mamlaka ya maandiko.
(n) Muhubiri, mwalimu au
mchungaji, anapofundisha Neno la
Mungu kwa uvuvio na ufunuo wa
Roho Mtakatifu na kunena Neno la
wakati, ujumbe huo ni wa kinabii.
Mgongano
Mara nyingi huduma ya nabii
hugongana na mchungaji kwa
sababu zifuatazo:
1.   Nabii husema Neno, pasipo
kujali hisia za wasikilizaji.
2. Mchungaji hujali hisia za
watu zaidi.
3. Nabii hutazama ujumbe
aliopewa, Mchungaji
hutazama watu
wanaosikia, inahitajika
hekima ya kukaa na
kuvumiliana. Katika kundi
mwenye neno la mwisho
ni mchungaji, hivyo nabii
ajizoeze kujitiisha kwa
mchungaji, wakati huo
huo mchungaji
asimdharau nabii.
4. Huduma ya nabii hufanya
kazi kirahisi kwenye timu
za kitume na kiinjilisti
zaidi ya kanisani
(Matendo 13:1-3).
5. Huduma hii haionekani
sana kwakuwa hatujatii
ipasavyo agizo kuu la
kuufikia ulimwengu na
injili.
6. Baadhi ya watumishi
husema huduma hii haipo
katika Agano Jipya. Huo
sio ukweli, huduma hii
ipo ila utendaji kazi wake
ni tofauti na Agano la
Kale. Ni hatari kanisa au
huduma kuwepo bila
ufunuo wa kinabii
kuwepo wakati wote kwa
njia ya Roho Mtakatifu.
Muhimu: Mengi niliyoandika
hapa yanatokana na
ufahamu wa maandiko na
uzoefu wa sehemu katika
huduma, maishani
mwangu na watumishi
niliowahi kuwasikia au
kuwafahamu kihuduma.

HUDUMA YA KINABII


Manabii
(Prophetes)
Neno nabii limetokana na maneno
haya “Pro ” yaani mbele, na
“ Phemi ” yaani kujulisha wazo la
Mungu au mtu, lisilojulikana.
Manabii husema mambo ya mbele
na pia ya sasa kwa uvuvio wa
Roho Mtakatifu. Kwa maana ya
pili niliyoisema hapo juu,
Mchungaji mwalimu au mwinjilisti
asemapo Neno wakati wa sasa kwa
msukumo na ufunuo wa Roho
Mtakatifu, asemapo Neno hilo la
wakati, husimama kama nabii kwa
wakati huo.
HALI HIZI IKIWA ZINADUMU
KWA MTU KATIKA HUDUMA
INAWEZEKANA NI NABII AU ANA
HUDUMA YA KINABII
(a) Nabii ni mtu awezaye kujua
wazo la Mungu la wakati na
kulisema au kulitenda.
Anaweza kuwa haitwi nabii,
lakini hali hii ni ya kinabii.
(b)  Nabii anapewa neema ya kujua
wazo la moyo wa mtu na
kulisema (Matendo 5:3). Mara
nyingine wazo la Mungu
kuhusu mtu, watu au hali ya
nchi na anga la kiroho.
(c) Mungu humpa kujua ayaonayo
Yeye (Mungu) wakati ujao,
wakati wa sasa au wakati
uliopita (Matendo 11:27-30).
(d) Manabii hutengeneza misingi
iliyoharibika na kuimarisha
misingi kwa njia ya kufundisha
neno la Mungu kwa ufunuo
wa Roho. Huduma ya
mwalimu afundishaye neno la
wakati kwa ufunuo wa Roho
inaweza kuitwa mwalimu wa
kinabii.
(e) Katika Agano jipya nabii
hufanya kazi katika timu ya
huduma, sio peke yake,
hufanya na viongozi wengine
katika huduma tano. Huyu
siye mtu mmoja aliyejuu na
wengine wote wako chini yake
wakisubiri Mungu aseme
kupitia yeye tu, mfumo huu
sio wa Agano Jipya. Katika
Agano Jipya manabii hufanya
kazi katika timu (Matendo
13).
(f)   Karama kuu katika huduma ya
nabii ni neno la maarifa,
unabii, neno la hekima,
kupambanua roho, mara
nyingine karama za nguvu
kama miujiza, uponyaji na
imani maalum. Kuna tofauti
kati ya huduma ya nabii na
karama ya unabii, mtu
akitumiwa katika karama ya
unabii haimfanyi yeye kuwa
nabii.
(g) Mara nyingine huduma ya
nabii hujificha katika huduma
nyingine. Kwa mfano mtu
anaweza kuwa mwalimu,
mchungaji au mwinjilisti na
hapo hapo ni nabii. Mfano wa
mtu wa namna hii ni askofu
Immanuel Lazaro.
(h) Manabii hupambanua nyakati
za kiungu na majira ya jambo
kufanyika na kuwaandaa watu
(Matendo 11:28, Matendo
21:10-11).
(i) Kila nabii ni mwombaji, lakini
si kila mwombaji ni nabii
(Yeremia 27:18). Haiwezekani
kuwa nabii bila kuwa
mwombaji, ila inawezekana
kuwa mwombaji bila kuwa
nabii.
(j) Utendaji kazi wa kinabii upo
tofauti tofauti. Kuna manabii
waalimu (Kenneth Haggin),
manabii wainjilisti(Charles
Finney), manabii wachungaji,
manabii mitume na manabii
walio manabii tu. Kuna
manabii waimbaji, pia
waombaji manabii. Wakati
wanaomba huona jambo na
kulibadilisha kwa mamlaka au
kulisimamisha kwa mamlaka.
(k) Neno la kinabii linaposemwa
ni vema lizalishwe katika
ulimwengu wa mwili kwa
maombi na maombezi, maana
adui hujaribu kuzuia kusudi
ka Mungu lililonenwa kinabii.
Mfano mtoto aliyetabiriwa
kuwa mtumishi, Neno hilo
latakiwa liatamiwe kwa
maombezi limtokee.
(l) Manabii na maneno ya kinabii
hujidhihirisha wakati maalum
( Kairos) na si wakati wote wa
masaa ishirini na nne
( Kronos). Katika Agano Jipya
huduma hii haionekani sana
pengine ni kwasababu ya
udhihirisho wa Roho
Mtakatifu na sauti ya Mungu
kwa kila mwamini.
(m)Nabii akitoa neno katika kundi
wajibu wake huisha. Wajibu
unaofuata ni wa mchungaji,
mwalimu au mtume kulithibitisha
na kulijaribu kwa maandiko na
kulihakikisha, hata kama ni Mungu
anasema (1Wathesalonike
5:20-21). Maandiko yana mamlaka
ya mwisho kuliko neno la kinabii.
Nabii lazima ajitiishe chini ya
mamlaka ya maandiko.
(n) Muhubiri, mwalimu au
mchungaji, anapofundisha Neno la
Mungu kwa uvuvio na ufunuo wa
Roho Mtakatifu na kunena Neno la
wakati, ujumbe huo ni wa kinabii.
Mgongano
Mara nyingi huduma ya nabii
hugongana na mchungaji kwa
sababu zifuatazo:
1.   Nabii husema Neno, pasipo
kujali hisia za wasikilizaji.
2. Mchungaji hujali hisia za
watu zaidi.
3. Nabii hutazama ujumbe
aliopewa, Mchungaji
hutazama watu
wanaosikia, inahitajika
hekima ya kukaa na
kuvumiliana. Katika kundi
mwenye neno la mwisho
ni mchungaji, hivyo nabii
ajizoeze kujitiisha kwa
mchungaji, wakati huo
huo mchungaji
asimdharau nabii.
4. Huduma ya nabii hufanya
kazi kirahisi kwenye timu
za kitume na kiinjilisti
zaidi ya kanisani
(Matendo 13:1-3).
5. Huduma hii haionekani
sana kwakuwa hatujatii
ipasavyo agizo kuu la
kuufikia ulimwengu na
injili.
6. Baadhi ya watumishi
husema huduma hii haipo
katika Agano Jipya. Huo
sio ukweli, huduma hii
ipo ila utendaji kazi wake
ni tofauti na Agano la
Kale. Ni hatari kanisa au
huduma kuwepo bila
ufunuo wa kinabii
kuwepo wakati wote kwa
njia ya Roho Mtakatifu.
Muhimu: Mengi niliyoandika
hapa yanatokana na
ufahamu wa maandiko na
uzoefu wa sehemu katika
huduma, maishani
mwangu na watumishi
niliowahi kuwasikia au
kuwafahamu kihuduma.

Alhamisi, 12 Machi 2015

JINSI GANI UTAELEWA KITABU CHA UFUNUO?


Jibu: La muhimu katika kutafsiri Biblia, hasa kwa
kitabu cha Ufunuo, ni kuwa na ufafanusi thabiti.
ufafanusi ni utafiti wa kanuni za tafsiri. Kwa maneno
mengine, ni njia ya kutafsiri maandiko. Ufafanusi wa
kawaida au tafsiri ya kawaida ya maandiko ina
maana kwamba kama mstari au kifungu
kinaonyesha wazi mwandishi alikuwa anatumia
lugha ya mfano, ni lazima ieleweke katika maana
yake ya kawaida. Sisi si hatustahili kuangalia kwa
maana nyingine kama maana ya asili ya msitari una
maana. Pia, sisi hatustahili kufanya maandiko kuwa
ya kiroho kwa kushirikisha maana kwa maneno au
misemo wakati mwandishi yu wazi, chini ya uongozi
wa Roho Mtakatifu, maana ieleweke kama
ilivyoandikwa.
Mfano mmoja ni Ufunuo 20. Wengi hutoa maana
mbalimbali kwa marejeo ya Kipindi cha miaka elfu.
Hata hivyo, lugha haimaanishi kwa njia yoyote
kwamba ushahidi wa miaka elfu moja kuchukuliwa
kwa maana ya kitu kingine chochote Zaidi ya kipindi
halisi cha miaka elfu moja.
Muhtasari rahisi kwa kitabu cha Ufunuo hupatikana
katika Ufunuo 1:19. Katika sura ya kwanza, Kristo
aliyefufuka na kuinuliwa anazungumzia Yohana.
Kristo anamwambia Yohana "kwa hiyo andika, yale
uliyoyaona, na yenye yako sasa na yatayofanyika
baadaye." Mambo Yohana alikwisha yashuhudia ni
kumbukumbu katika sura ya 1. "Mambo ambayo
yalikuwa" (yaliokuwapo katika siku ya Yohana) ni
kumbukumbu katika sura ya 2-3 (barua kwa
makanisa). "Mambo yatakayofanyika" (mambo ya
baadaye) ni kumbukumbu katika sura 4-22.
Kwa ujumla, sura ya 4-18 ya Ufunuo inazungumzia
hukumu ya Mungu juu ya watu wa dunia. Hukumu
hii si kwa ajili ya kanisa (1 Wathesalonike 5:2, 9).
Kabla ya hukumu kuanza, kanisa itakuwa
imeondolewa kutoka dunia katika tukio liitwalo
kunyakuliwa (1 Wathesalonike 4:13-18, 1
Wakorintho 15:51-52). Sura ya 4-18 huelezea
wakati wa "shida ya Yakobo" -matatizo kwa ajili ya
Israeli (Yeremia 30:7; Danieli 9:12, 12:1). Pia ni
wakati Mungu atawahukumu walio kufuru kwa
sababu ya uasi wao dhidi yake.
Sura ya 19 inaeleza kurudi kwa Kristo na Kanisa,
bibi harusi wa Kristo. Akiweza mnyama na yule
nabii wa uongo na kuwatupa wao katika ziwa la
moto. Katika sura ya 20, Kristo anamfunga Shetani
na kumtupwa katika shimo la kuzimu. Basi, Kristo
anauansisha ufalme wake hapa duniani ambao
utadumu miaka 1000. Mwishoni mwa miaka 1000,
Shetani atafunguliwa na anaongoza uasi dhidi ya
Mungu. Yeye kwa haraka anashindwa na pia
kutupwa katika ziwa la moto. Kisha hukumu ya
mwisho hutokea, hukumu kwa makafiri wote, wakati
wao pia watatupwa katika ziwa la moto.
Sura ya 21 na 22 hueleza kile kinajulikana kwetu
kama hali ya milele. Katika sura hizi Mungu
anatuambia namna milele pamoja naye itakuwa.
Kitabu cha Ufunuo kinaeleweka. Mungu hangeweza
kupeana hicho kitabu kwetu kama maana yake
kamwe ilikuwa siri. Muhimu katika kuelewa kitabu
cha Ufunuo ni kukitafsiri kijuu juu iwezekanavyo-
kinasema chenye kinamaanisha na kumaanisha
chenye kinasema.

Ijumaa, 6 Machi 2015

MITUME

Katika Agano Jipya tunaona mitume wakitajwa kama mara 80 hivi, kwahiyo kwa vyo vyote katika kanisa la kwanza walikuwa ni watu muhimu, na kwa kweli ~ Mitume ni ‘wa kwanza’ kanisani (1Kor 12:28). Kanisa limejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii (Efe 2:20). Mitume na manabii wana ufunuo maalum na uwezo wa kuelewa mambo kutoka kwa Mungu (Efe 3:5) (Yud 1:17). Makanisa yanapaswa kuwa na mitume wao (2Pet 3:2).

Lakini je, mitume ni kwa ajili ya siku zetu pia au walikuwepo mwanzo kwa kazi ya kuanzisha Ukristo?

Kama hata sasa wanatakiwa, ni akina nani hao na wanafanya nini? Sisi Tunafanya Nini?

Leo hii tunaongozwa mara kwa mara na watawala au wachungaji wenye karama, lakini kama mitume bado ni ‘wa kwanza’ wa Mungu katika kanisa na moja ya  misingi yake, tunapaswa kufanya nini?

Mtume Ni Nani?

Neno Mtume lina maana ya mtu anayetumwa, na kupewa uweza wa kufanya umisheni kutoka kwa Mungu. Utume si cheo, ni wito, ni karama na shughuli kama shughuli nyingine yo yote ndani ya kanisa. Mitume Katika Agano Jipya Yesu, yu juu ya wote, (Ebr 3:1). Wale mitume thenashara wa Mwanakondoo (Mk 3:14-16) (Mdo 1:26) (Ufu 21:14). Karama ya mtume (Efe 4:11); watu kama Paulo, Yakobo, Barnaba, Timotheo, Sila, Andronika na Yunia. Biblia haijatuambia kwamba hawa walikuwepo kwa ajili ya karne ya kwanza peke yake. Kutokana na ukweli kwamba Kristo aliweka wengine kanisani kuwa mitume  ili kutenda kazi ambayo bado haijakamilika (Efe 4:12-14) ni ushahidi tosha kwamba mitume wanahitajika sana hata leo kama karama nyingine zilizozoeleka zaidi (Efe 4:11).

Ni Nini Kazi Za Mtume?

Si kila mtume anayetenda kila kazi kama inavyoonekana katika Agano Jipya lakini kazi za kitume ni pamoja na ~

Kueneza injili, kwa mfano safari nyingi za Paulo, na ziara ya Petro kwenye eneo lile ambalo halikuwahi kufikiwa kabla katika nyumba ya Mmataifa (Mdo 10). Kuwafikia watu ambao hawajafikiwa (Rum 15:20). Kusababisha uinjilisti mpya kufanyika (Mdo 19:10). Kusababisha makanisa mengi mapya kuanzishwa, kama alivyofanya Paulo kusini mwa bara la Ulaya. Kuwa mjenzi mkuu mwenye hekima, anayejua la kufanya (1Kor 3:10; 5:3; 6:4; 7:1; 8:1).   ®Mitume Huweka Misingi Imara Ya Kristo (1Kor 3:11) Ya maisha katika Roho (Mdo 19:1; 8:14-17). Ya utii mbele za Mungu (Rum 1:5). Ya fundisho la kweli (Efe 3:2-21) Ya viongozi wazuri (Mdo 14:23) (Tit 1:5).
®   Kuwa baba au mama wa makanisa machanga, kuyatia moyo kwa nyaraka na ziara, na kamwe si kuyadhibiti (2Kor 11:28) (1The 2:7,11).
® Kukabiliana na tamaduni zisizo na maana, kama Paulo alivyopingana nazo hata kwa Petro (Gal 2:11-14). Safari za kuuunganisha Mwili kama alivyofanya Paulo akiunganisha Yerusalemu, Antiokia na makanisa  mapya kwa mahusiano yake.   Alionesha urafiki wa muda mrefu na uaminifu, akitenda kazi katika mahusiano na si katika mifumo na vyeo (1The 1: 5-7; 2:8) (Flp 1:8; 4:10,14,15) (Mdo 20:31; 18:11).

Utamtambuaje Mtume?

Mitume huitwa na Mungu, na wakajua, na watu wote pia. Wanaweza wakakubali wito wao, lakini hawana haja ya kutangaza nafasi yao kama cheo, na haipaswi kuwa hivyo, badala yake ni nafasi yenye majukumu makubwa. Angalia salamu za Paulo anavyoanza kuandika nyingi ya nyaraka zake; na pia angalia uone kwamba mitume ~ Wanatambuliwa na viongozi wengine wa kanisa (Mdo 15:2,4). Wanatenda kazi na kuonesha ushuhuda wa wito wao si kwa kulazimisha na kudhibiti wengine, bali kwa kuendelea kuweko udhihirisho wa uweza wa Roho (2Kor 11:6-13). Wanao watu kama uthibitisho hai wa huduma yao (2Kor 3:2,3). Wamepakwa mafuta kwa ajili ya huduma (2Kor 12:12). Wamemwona Mungu wao wenyewe katika historia ya ustahimilivu katika shida na upinzani (2Kor 12:7-10) (1Kor 4:9-13). Mitume Pia

•Wanahitaji Makwao

Mitume katika Agano Jipya wanaonekana sikuzote wakitenda kazi katika timu ya umisheni au pamoja na wazee wa kanisa nyumbani ambako ni kituo cha kitume Angalia Matendo 15 na somo la 12.

•Ni Nini Kituo Cha Kitume?

Ni kanisa la mfano, ambako mitume, timu mbalimbali na watu wanakusanyika pamoja kwa ajili ya Yesu na kwa ajili yao wenyewe kwa wenyewe. Ni mahali pa kuanzia na kituo cha kupatia watu, fedha na vifaa kwa ajili ya umisheni. Ni mahali pa ushirika, pa kuhuishwa, pa kuwajibika na kuwategemeza wale wanaofanya huduma za kitume, na kamwe isiwe piramidi ya huduma yenye ‘mtume aliyewazidi wenzake’ akiwa kwenye nafasi ya juu akitoa amri tu. Ni pale tu timu ya Paulo ilipokuwa nje ya kituo huko Antiokia ndipo walipojitawala na kujitegemea (Mdo 14:26-28).

•Vituo Vya Kitume Katika Biblia•

Makanisa ya Yerusalemu, Antiokia, Efeso na Thesalonike yalikuwa ni zaidi ya makanisa ya maeneo tu. Haya yalikuwa na huduma katika Roho Mtakatifu yakifanya maombi, uinjilisti, unabii, mikutano ya mafundisho na ibada. Kulikuwa na viongozi kadhaa, kanisa lililo hai na ushirika. Walikabiliana na changamoto za kisheria, mateso, mkakati na kupeleka timu za kitume na kuusaidia ulimwengu wa Wayahudi, na kuendelea hadi Samaria na hatimaye kwa mataifa.  

•Ni muhimu kwamba mitume wajifunze nyumbani na kisha wawapelekee wengine hayo masomo. Ni lazima vituo vya kitume vifaulu mtihani wo wote, na pawe ni mahali ambapo timu za kitume zinaona fahari kuelekeza watu na kuwakaribisha kuja kujifunza.