Jumamosi, 15 Agosti 2015

ELIMU/MAFUNDISHO YA MASHETANI.

Bwana YESU Asifiwe wana wa MUNGU leo imempendeza BWANA kujifunza somo hili linalohusu mafundisho ya mashetani.

NINI MAANA YA ELIMU/MAFUNDISHO YA MASHETANI?

Mafundisho ya mashetani ni mafundisho yanayofundishwa kinyume na mafundisho ya kweli ya kristo. Walimu wanaofundisha haya wanafundisha kinyume na injili ya kweli na huonesha wazi wazi kuwa kristo bado hajatutoa dhambini yaani hutufanya tujione bado sisi tuaminio hatujaamini au yanaonesha kazi ya msalaba kuea haijakamilika bado.  1timotheo  4:1-4 "  "

Biblia inasema  siku za mwisho watu watajitenga na imani ya kweli na kufuata mafundisho ya mashetani na biblia inaposema mafundisho ya mashetanihaimanishi kuwashetani au mashetani yanakuja yenyewe kufundisha bali yana watu wanaofanya kazi hiyo. Kumbuka watu  hujigeuza yaani wamejifanya kama watumishi watakatifu wa Mungu aliyehai..kumbuka watumishi wa ibilisi hujigeuza wafanane na watumishi wa kweli sio kwamba ndivyo walivyo bali wamejigeuza tu wawe mfano wa watumishi wa kweli ila sio halisia.

CHANZO CHA MAFUNDISHO YA MASHETANI
Mafundisho haya yanatokana na vyanzo hivi vifuatavyo.

1…Chanzo kwanza kabisa ni  ROHO ZIDANGANYAZO 1timoth 4:1
" Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati
za mwisho wengine watajitenga na imani,
wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya
mashetani
Roho hizi wakati mwingine huitwa roho mbaya na hii roho zina uvuvio wa pepo wachafu..kumbuka kuwa
"Roho ina uwezo wa kumsemesha mtu na kumwaminisha juu ya jambo fulani.Na kumfanya mtu aamini vilevile;
roho hizi ndizo hufanya kazi ya kutoa utabili wa uongo na huweza kuja kwa ndoto maono au kukusememesha kimya kimya.  yoh  8:43... .
8:43
" Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba
yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa
mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika
kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake.
Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe;
kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.
biblia inatueleza kuwa shetani ndiye mwanzilishi wa uongo na ndiye baba wa huo kwa hiyo utambue roho yake hufanya hayohayo, mhimu ujue hivi roho ya ibilisi hufanya uvuvio juu ya watu wake na huyatetanda mambo yao kwa nguvu ya huyo bila wao kujua..

NITAENDELEA

Jumatatu, 10 Agosti 2015

JE UNADHARAULIWA?

Watu wengi waliobeba Kusudi la Bwsna siku zote wamekuwa na changamoto ya kudharauliwa ktk yale wanayofanya;jambo hili limewavunja moyo wengi;limewatoa watu sana kwenye makusudi na kufanya washindwe kuendelea ma kile walichokuwa wamekusudiwa na Mungu

Nehemia    4:
1 Lakini ikawa, Sanbalati aliposikia ya kwamba
tulikuwa tukiujenga ukutuha, akaghadhibika, akaingiwa
na uchungu sana, akawadhihaki Wayahudi.
2 Akanena mbele ya nduguze na mbele ya jeshi la
Samaria, akisema, Wayahudi hawa wanyonge
wanafanyaje? Je! Watajifanyizia boma? Watatoa
dhabihu? Au watamaliza katika siku moja? Je!
Watayafufua mawe katika chungu hizi za kifusi,
nayo yameteketezwa kwa moto?
3 Basi Tobia, Mwamoni, alikuwa karibu naye,
akasema, Hata hiki wanachokijenga, angepanda
mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe.

Shetani ana watu aliowaandaa kupinga au kuzuia kusudi pa Mungu hawa hupenda kuonesha kuwa wewe ni dhaifu sana na hauwezi ktk unalolifanya.

Unaweza kukutata na kikwazo hiki..adui yako kuona kazi yako ni dhaifu kuliko uhalisia wenyewe..rejea kauli ya tobia.

na wewe umekutana akina tobia wengi wao kazi yo ni kuvunja moyo na kuonesha kushindwa kuliko kushinda;wanapenda kukutiisha kwa vitisho na hata kukutungia mabaya..hakika hii ndiyo siri ya waovu kukuchimbia shimo ile ufe..

Lkn tambua hili wewe ambaye  alitenda kusudi ni wa maana sana;wewe umebeba dhamana na uhai wa jamii,taifa na familia yako ..wewe ndiye utaleta badiliko juu ya eneo hilo kiroho na kimwili ;usiogope wala kukuta tamaa shikilia tu neno la BWANA utafanikiwa;

Usiangangalie ziaka na dharau zao amini tu umebeba kitu cha thamani usikishushe njiani mpaka ufikishe mahali husika

Ni vigumu kujiamini wakati jamii,na watu na ulimwengu wanakuambia maneno na yanayoonesha dharau ya dhahiri kwenye maisha yako, lkn neno la Mungu linatuambia hivi USIOGOPE  isaya 43:1-4.
1 Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo,
yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope,
maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako,
wewe u wangu.
2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe;
na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika
moto, hutateketea; wala mwali wa moto
hautakuunguza.
3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa
Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa
ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili
yako.
4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na
mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa
sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za
watu kwa ajili ya maisha yako.
5 Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta
wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka
magharibi;
Dharau imeficha utukufu nyuma yake ,ukisoma neno hapo juu tugundua haya.

1®Wewe una kundi kubwa nyuma yako.
Bila kutambua hili watu wengi wanakata tamaa bila kujua kuwa kuna watu wengi wako nyuma yao kwani dharau ni jaribu linalokuja ili kukupima kama unaw eza kuongoza au la,kumbuka musa,alidharauliwa. YESU alidharauliwa na manabii wote walidharauliwa.

2®Wewe una vitu vya kipekee ..maana nyingine ni kwamba una vitu vya kipekee na tofauti na wengine.

Ukiangalia Mafarisayo walimwona YESU kama mtoto asiyehitaji heshima yao;wakamdharau kwa kuwa hakuwa na mambo kama yao bali alikuwa na hekima tofauti na hekima ya kifalisayo;ukiwa wa tofauti mwanzoni lazima udhalauliwe;utainekana mtu usiyefaa kwani wewe unalevel ambazo hazifanani na za kwao

wewe ujue hili Yesu aliyekuita anakutamvua usihangaike na mwanadamu songa mbele Bwana yuko pamoja nawe.

Alhamisi, 6 Agosti 2015

MAOMBI YA KUOMBEA UCHAGUZI WA TAIFA

Bwana asifiwe sana..leo ninahimizwa nianze kufundisha somo lisemalo..

MAOMBIYA NAMNA YA KUPATA VIONGOZI WA TAIFA KTKA KUSUDI LA MUNGU..

Kabla ya yote napenda kusema hatuwezipata viongozi kama hawakuchaguliwa na 18
Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya
wakuu.
19
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa
nguvu; Na mashindano ni kama mapingo ya ngome na Mungu  pili na mwanadamulkn ktk yote huwezi kuchagua kama hakuna watu zaidi ya mmoja..Mfano Mungu ametuchagua sisi kutoka ktk watu wengi wa duniani ili tuitwe wanaye.

Kwa habari ya uchaguzi wa taifa lolote unapozungumza uchaguzi ni kama mshindano....NINAPENDA NISEME...Mambo ya Uchaguzi ni mpango wa Mungu vs usio wa Mungu..
Ninamaanisha wako wa MUNGU pia wako hawatokani na mpango wa MUNGU.MITH. 19: 18
Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya
wakuu.
19
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa
nguvu; Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.

Mistari hii inaonesha kuna team mbili yaani Mpango wa Mungu vs mpango usio wa MUNGU ..Sasa wengi hatukati haya mashindano vizuri kwa kudhani Mungu hausiki hapa;wakati wa sauli tunaona watu walitaka Mungu awape mfalme wa kuwatawala lkn kumbe Mungu hakutaka afanye hivyo muda huo.sasa huo ukawa mpango wa Mungu vs mpango wa shetani..

Mungu ndiye huwaweka watawala juu ya nchi na wala si mwadamu

JINSI GANI YA KUOMBEA UCHAGUZI WA VIONGOZI

Kwanza tambua lazima uombe kwa kanuni zifuatazo

1:  Maombi ya toba ni mhimu ..
Maombi haya yatahusu taifa ;viongozi waliotangulia ;ardhi na mipaka ya nchi..
imeandikwa... ISAYA 64:6  "Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu;na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo uliyotiwa unajisi;sisi sote twanyauka kama jani;na maovu yetu yatuondoa,kama upepo uondoavyo"

Hakika tumekaa ktk taifa lenye dhambi sisi pia tumehesabiwa na na wasiohaki tumechafuka kwa kuwa sisi ni walinzi kiroho na hatufanya wajibu wetu kama waombaji..hatukuwakemea mafisadi  sasa MUNGU aturehemu ktk haya yote.

Tunatubu kwa kuwa kuna mikataba imefanyika kinyume na ufalme wa MUNGU...  ISAYA  28:1-18

"....lisikieni neno la BWANA enyi watu wenye dharau;mnaowatawala watu haea walio ndani ya Yerusalemu.Mmesema tumefanya agano na mauti ;tumepatana na kuzimu......"

Tunahitaji kutubu kwani watawala wamekubaliana na kuzimu yaani walipokuwa wanaingia madarakani walienda kwa wachawi ili wawasaidie kumbe hapo wamejiunganisha na kuzimu bila kujua..ukiendelea kusoma inasema umefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio ...sasa unatakiwa ujue kuna watawala hujiamini lkn kujiamini kwao ni kwa sababu mganga wao anawahakikishia mambo mazuri..ni kwa kuwa kuzimu inawapa nguvu..

unaweza usinielewe lkn nikwambie wengine wanatawala kwa kafara .sasa ujue wewe umewekwa kubatirisha mambo hayo.
DAMU YA YESU NDIYO SILAHA HAPA.

KESHO NITAELEZA KIFUPI NA JINSI YA KUFANYA MAOMBI HAYA YA TOBA..   

bishop eliya kasebele..

SIMAMA MAHARI PALIPO BOMOKA
KUJENGA..

Revival builders church..
PO BOX     140

RUVUMA-TANZANIA
EAST AFRICA
EMAIL..emanuelkasebelee@gmail.com
+255766891120