AGANO
kusoma sehemu ya 3 na 4 ya somo hili
wiki iliyopita basi BONYEZA HAPA kabla
hujaendelea na sehemu ya 5 na 6. Barikiwa
SEMINA YA MWL MWAKASEGE DODOMA
SOMO: FAIDA ZA KUTEMBEA KATIKA BARAKA ZA
AGANO NA MUNGU.
Neno kuu: Eph 1:3
DAY FIVE.
Utangulizi: Luk 22:20, Ebr 8:6
•Maana ya Bora( agano): lenye uepesi wa kutumia
agano ili kufikia kusudi la agano lililowekwa. Math
5:17-19, Ebr 8:7,13
•Maana ya kuukuu: matokeo ya kitu kutoweza
kuhimili matumizi. Inaweza kusababishwa na:
•Ongezeko la matumizi bila kupumzishwa/
Matumizi ya mara kwa mara
•Cha zamani hakiendani na hali ya wakati wa sasa.
•Kuna uhusiano kati ya agano jipya na maagano
yaliyopita.
•Agano jipya limekuja kuyakakamilisha maagano
yaliyopita. Ndani yake limebeba upatikanaji wa
maagano yaluyotangulia.
•Huwezi pata maagano yaliyopita bila agano jipya.
CHANGAMOTO TULIZONAZO LEO
1. Kutoyatazama maagano yaliyotangulia kwa jicho
la agano jipya.
2. Kutokujua namna ya kutumia kilichopo ndani ya
agano jipya ili kupata yale yaliyomo katika
maagano yaliyotangulia
Agano la Ibrahim
Gal 3:13,14,29
Baraka ya Ibrahim na ahadi alizohaidiwa.
Mwa 24:1,34,35
•Alibarikiwa katika vitu vyote.
Mwa 12:2, 22:17
Kumiliki lango la adui wako. Mwa 15:18-19
•Haiwezekani uzao wake kutomiliki aridhi/ nchi.
Rom 4:13. Hii ni ahadi ya Ibrahim.
Agano la Sinai
Gal 3:13-14.
•Kristo alikufa msalabani ili tuipate baraka ya
Ibrahim.
Gal 3:16-29
•Kilichopatikana katika agano hili ni kutengenezwa
kwa hema ili Mungu apate maskani.
•Mungu alikuwa akiachilia ufalme wake kwa
wanadamu.
•Ndani ya sheria kukatokea ukuhani au agano la
Lawi.
•Wazaliwa wa kwanza kupata heshima yao.
Chakula cha Bwana ni sehemu ya agano. Luk
1:31-32, Ufu 3:21.
Agano la Daudi
•Mungu aliteremsha kiti cha Mfalme.
•Yerusalem ni mji wa Mfalme mkuu.
Agano la Jerusalem
•Mungu anaweka hekima kwa wanadamu kusema
juu ya Yerusalem. Mwa 6:18.
DAY SIX
Utangulizi:
Swali: Unazipataje hizo baraka za agano?
Gal 3:13-14
•Kazi ya msalaba ni kutoa nafasi kwa watu wasio
wayahudi( mataifa) kupata baraka na ahadi ya
Ibrahim kupitia Kristo.
Rom 8:16-17, Gal 3:29
•Ukitaka kurithi baraka za Ibrahim ni lazima uwe
mrithi wake
HATUA ZA KUKUSAIDIA KUONA BARAKA
ZINATOKEA KATIKA MAISHA YAKO NA
UNATEMBEA NAZO.
1. Zaliwa mara ya pili ili uwe mwana wa Mungu.
Eph1:3, 4,5,11,13,14
2Cor 5: 17, Yoh 3:3
•Sisi tulio wa mataifa ni lazima tuzaliwe mara ya
pili ili tuwe warithi wa Ibrahim.
•Kama haujaokoka ni lazima uokoke.
2. Fahamu ya kuwa kwakuwa wewe ni mwana wa
Mungu ni mrithi pamoja na Kristo.
Gal 4:6-7, Rom 8:16-17, Luk 15:11-32
•Ili upokee baraka ni lazima ujue ya kuwa wewe ni
mrithi. Eph 1:13-14
•Kazi ya Roho mtakatifu ni kutushuhudia.
3. Omba maombi yanayohusu urithi wako.
•Mungu akujulishe na kukuonesha urithi ulionao.
Efe 1:17-18
Tujue utajiri wa utukufu wa urithi wake katika
watakatifu wake.
•Ufalme wa mbinguni ni urithi wako. Math 25:34
•Uzima wa milele ni urithi wako. Math 19:29
•Baraka ndani ya ndoa. 1Pet 3:7-9
•Wenye hekima kurithi utukufu. Mith 3:35
•Mbinguni ni urithi. 1Cor 15:50-56
•Malaika kukuhudumia ni urithi wako. Ebr 1:14
•Jina la Yesu ni urithi wetu. 2Nya 7:14
•Aridhi ni urithi wetu. Kuna mahali Mungu
amekupangia kurithi. Ebr 11:8
•Omba akupe huo urithi uwe wako. Mdo 20:32, Zab
2:7-8
4. Ukue katika Kristo usibaki mtoto. Gal 4:1-3, Col
1:13
•Uaminifu
Luk 16:10-12
Usipokuwa mwaminifu Mungu alipokupa kufanya
huduma na mtu mwingine hutapewa huduma yako
mwenyewe.
Mith 28:20, Mith 23:7, 1Cor 13:11, 3:1-9, Yoh 15:15,
Ayu 22:21, Zab 133:1-3, Efe 4:11
Litaendelea…..
